KATIKA Mpango wa Kimkakati [Strategic Plan] kwa kawaida taasisi huwa inaangalia pale ilipo na kule inakotaka kwenda na kuwepo baada ya miaka kadhaa!
Hii ni determination ya kile kitu tunachokiita VISION, MISSION AND VALUES FOR THE ORGANIZATION OR INSTITUTION OR COUNTRY na kwa leo hapa ni hii nchi inayoitwa TANZANIA!
Swali la kujiuliza hivi Tanzania inaisheshimu Vision iliyojiwekea yenyewe sikumbuki tarehe lakini ninaamini wakina kaka Mwapachu na wenzake walifanya kazi nzuri tu, japo kwa leo kuna mambo yanaweza kuwa yamepitwa na wakati! Au yanastahili kuongezwa mengineyo kutokana na kasi ya mabadiliko inayosababishwa na hali ya kiuchumi ya dunia, utandawazi na teknolojia!
Baada ya kuwa na VISHENI hiyo sasa wanasiasa wanatuambia nini kuhusu nini visheni ndogo na wizara na MISSION au AZMA za wizara na mikoa mbalimbali na viongozi mbalimbali wa kijamii na kiuchumi!
Na je kwa utamaduni, maadili yasiyo maadili na tabia zetu hizi zinazoitwa za Kiswahili tunaweza kutekeleza visheni na azma hizo?
Mimi ninaamini bila kuwa na maadili ya Kitanzania yanayojulikana na kuheshimika ulimwenguni kote basi itakuwa ni shida sana kutekeleza kazi iliyo mbele yetu.
Ni lazima Watanzania tuzungumze. Tuzungumze tunastahili sisi na vizazi vyetu kuwa ni watu wa namna gani?
Je, tunastahili kuheshimu na kuhifadhi tamaduni na lugha za makabila yetu ya asili na kuifanya lugha ya Kiswahili ndio utamaduni na lugha peke?
Je, tunastahili kujifunza lugha nyinginezo? Ni lugha zipi hizo na kwa sababu gani na zitatusaidia vipi kuongeza maarifa na kupunguza ujinga na pengine kutuwezesha kuvuta wawekezaji wa aina fulani?
Je, tunataka kuwa watu waaminifu na watenda haki au kuwa watu wasio na uaminifu na wanaobufu fedha tu wakati wote?
Je, tunaweza kuamua kuwa taifa linalojali usafi kuanzia chooni hadi Ikulu? Au ni taifa ambalo kampuni za wazoa taka ni za ndugu na shemeji wasio na uwezo wa kuendesha biashara hizo?
Je, tunataka tusifike kwa uchapaji kazi au kwa ulegevu na uvivu?
Je, tuanweza kuwa taifa linalojali wakati kama rasilimali isiyorudishika au watu wasiopenda kufungwa na wakati na mtu anaweza kuja kwenye kikao wakati wowote anaopenda?
Je, tunaweza kuwa taifa la watu wanaoheshimu ndoa na familia zao au la wazinzi na watumiaji kondomu maana tatizo sio zinaa ila ni ukimwi?
Je, tunataka kuwa taifa la watu wanaothamini elimu na maarifa au taifa la wababaishaji ambalo hata mawaziri na wabunge wanaishia kusoma magazeti ya Ijumaa, Uwazi na Kiu?
Je, tunataka kuwa taifa lenye aibu na haya au taifa la watu wasiokereka kuona watu wanatembea nusu uchi au hata uchi wa mnyama kabisa?
Je, tunataka kuwa taifa la watu ambao kiongozi asiyechangia maendeleo yao na ya nchi anabakia tu ofisini au taifa la watu ambalo mtu lazima aoneshe kustahili kubaki kwenye ofisi fulani?
Je, tunataka kuwa na nchi ambayo wizara zote zimekusnywa mahala pamoja dar es salaam na wala sio makao makuu ya nchi tarajiwa au nchi ya watu ambayo wizara zinajengwa kwenye mikoa au kanda ambazo huduma zake zinazohitjiaka zaidi?
Je, tuwe ni nchi inayotegemea misaada kwa maendeleo yake au tunaojua thamani ya rasilimali zetu na kuziuza kwa bei nzuri ili kiasi cha fedha za maendeleo zinazohitajika kila mwaka zipatikane kila siku?
Je, tuwe na nchi ambayo vyanzo vya mapato ya vyama vyake vya kisiasa ni siri au nchi ambayo kila shilingi chama cha kisiasa inayoipata inajulikana imetoka wapi?
Je, tuchanganye biashara na siasa au siasa iendeshwe na wanasiasa na biashara na wafanyabiashara?
Je, tuwe taifa la watu wanaokataa maovu na kutunuku mema au kinyume cha hivyo?
Je, tuwe taifa la watu waongo au watu wanaothamini ukweli mbele ya cheo au mali?
Haya ni baadhi ya maswali yanayopaswa tujiulize ili tuje na tamko la maadili ya kitaifa. Sio jambo la kuamuliwa siku moja na mtu moja bali linalohitaji mchakato ambao unashirikisha vyombo vyote vya habari, kulia na kushoto, ili hatima ya yote yapatikane aina ya maadili ambayo kila Mtanzania atajivunia kuwa ni maadili yake!
Vinginevyo nchi isiyo na maadili ina hatari ya vijana wake kuwa bendera fuata upepo. Vijana hao ambao wengi ni kama sponchi ni wepesi wa kunyonya hata mabaya, maovu na machavu na yanayotia kinyaa kama vile ni kitu cha kistaarabu, maendeleo na c ha kujivunia kumbe ni kinyume cha hivyo. Mwisho wa yote kijana anachanganyikiwa inakuwa ni hasara kwa familia na taifa!
Tuwaokoe watoto na kizazi cha nchi hii kwa KUWA NA KONGAMANO LA MAADILI YA KITAIFA litakalotoa TAMKO LA HAYA NDIO MAADILI YA MTANZANIA!
Tuesday, September 2, 2008
Subscribe to:
Posts (Atom)
