KUNA tabia iliyojengeka miongoni mwa Watanzania kwa baadhi yao kujiona bora na hivyo kuona kwamba nafasi au vyeo vya chini katika uongozi sio laiki yao. Kwa sababu wenzetu hao wanajiona wamesoma sana, matajiri sana au wana vyeo vikubwa sana basi wanawaachia watu wasiosoma, masikini na wanyonge nafasi za uongozi katika ngazi za chini kama vile usimamizi wa nyumba kumi, ukatibu kata, uenyekiti wa mitaa na udiwani. Wao wote wanakimbilia kuwa wabunge, wawakilishi na maraisi japo wanajua fika nafasi hizo ni chache mno na kwamba uongozi si lazima uwe mbunge au waziri au rais wa nchi. Chukulia mfano wa Zanzibar kuna wagombea wengi tu ambao wangelifaa kuwa wakuu
Funzo ambalo ningelipenda lijulikane asubuhi na mapema na dhamira kuu ya insha hii ni kwamba bila kuwa na viongozi walioelimika, walioridhikia kimaisha na wanaojua kutofautisha kati ya kutumiwa na viongozi na kuongoza wenyewe nchi hii haitaondokana na umasikini wa kutupwa kwa miaka mingi ijayo.
Kwa maneno mengine, mapinduzi ya kweli ya kiungozi yatakuja tu pale tutakapokuwa na viongozi wa ngazi za chini wanaojua uongozi, uchumi, nadharia tofauti za njia, mbinu, mikakati ya maendeleo na elimu zinazoendana na masuala kama hayo. Hawa watakuwa ni viongozi wanaoweza kuunda baraza la mawaziri la mkoa na ambao wanaweza wakahoji maamuzi yanayofanywa na bunge la taifa na baraza la mawaziri la taifa kwa kuwa wana elimu sawa na walioko juu, ingawa wao zaidi ni katika lugha mama ya taifa, Kiswahili.
Isitoshe uongozi wa namna hii ukipatikana katika ngazi ya chini kabisa itakuwa ni rahisi kutathmini viongozi na kuwapa dhamana kubwa zaidi kulingana na mafanikio yao katika ngazi za chini.
Chini ya Uongozi wa kijamaa Watanzania wengi waliokuwa na elimu, vyeo na mali walikataa katakata kugombea nafasi za ujumbe wa nyumba kumi,udiwani na uongozi wa mitaa. Ikawa ni kawaida kwa nafasi hizo kuchukuliwa na watu wasiokuwa na elimu au wenye elimu ndogo sana; wasiowahi kushika cheo chochote na waliokuwa wanaongoza kwa umasikini na hali ngumu ya maisha katika mitaa yao.
Hali hiyo ukienda leo kwenye mikoa mbalimbali na hasa huko vijijini bado ipo na inaendelea. Swali la kujiuliza ni kwamba ikiwa familia, mitaa na vijiji ndio msingi au matofali ya msingi ya taifa leltu hivi kweli tunaweza kujenga taifa lililo imara kisiasa na madhubuti kiuchumi, kijamii, kitekonoojia na kijeshi endapo uongozi wake unashikwa na watu sampuli hii ?
Ieleweke kwamba siwadharau hata kidogo wale walioshika dhamana hii pale ambapo matajiri, wasomi na watu wengine wenye majina walipoidharau na kuikataa. Ila kutokana na mabadiliko ya wakati ambapo sasa Tanzania ni sehemu tu kiuchumi katika ulimwengu mkubwa zaidi naona upo umuhimu wa kujitazama na kujipanga upya ili tuweze kuzikabili changamoto mbalimbali za maendeleo zinazotukabili.
Pengine kuna kosa la kiufundi lililofanyika katika ugawaji dhamana na maslahi yanayoendana na hili. HIvi anayestahili kulipwa mshahara mzuri ni kiongozi wa ngazi ya chini kabisa (ambaye anaweza kuibadili hali ya watu wake toka umaskini au daraja la tatu wakawa la pili au la kwanza) au kiongozi wa ngazi ya juu ambaye nadra kuwa na mawasiliano na wananchi huko waliko?
Ukweli ni kuwa viongozi wetu wa nyumba kumi, wenyeviti wa mitaa na makatibu kata wote elimu yao, uzoefu wao, uono wao na ufahamu wao wa dunia ya utandawazi bado uko chini kwa upande mmoja. Na kwa upande wa pili maslahi na motisha yao ya kuleta mabadiliko ya kimsingi katika jamii zao ni sawa na hamna au ni kidunchu mno. Hii haina tofauti na mameneja, makocha na viongozi wengine wa timu ya michezo kulipwa mara kumi au ishirini ya wachezaji halafu timu ikawa inadorora mwaka nenda, mwaka rudi -halafu unatafuta mchawi nje yenu !
Viongozi au watu wanaoitwa viongozi katika ngazi za chini kwenye nchi hii ni watu wasiolipwa mishahara; hawana elimu ya kutosha kuongoza na kuleta mabadiliko katika jamii; hawana ari, motisha wala moyo wa kufanya kazi; hawana ujuzi na uzoefu katika kazi wanazozifanya na wala hakuna taasisi iliyojipanga au kupangwa kuwafunza na kuwaendeleza.
Viongozi hao wa chini wengi ni masikini kiasi cha kutisha kiasi ambacho sio tu wana vishawishi vingi bali pia wanakuwa sio amana bali deni kwa taifa na hasa pale wageni toka nje ya eneo lao au nje ya nchi wanapokuja na kitita cha fedha na kuwashawishi zaidi. Au wanapotishwa na viongozi wa ngazi ya kitaifa hadi kuwadhulumu na kuwaonea watu wao wenyewe.
Hata tupate viongozi wa kitaifa ambao wote ni maprofesa lakini huku chini tuna watu wasiosoma, masikini na wenye ujuzi sawa na hamna katika masula ya uchumi, biashara, uwekezaji, ujasiriamli, menejimenti, usimamizi wa fedha, sheria na kadhalika nchi yetu haiwezi kamwe kuendelea.
Tutajenga kama mataifa mengine yaliyopotea kizazi cha viongozi wanaorithiwa na watoto wao mwaka nenda, mwaka rudi. Ni mwanzo wa kuwa na nchi ambayo itakubali na itaendelea kukubali uongozi mbovu kwa sababu mfumo uliopo hauna chachu wala changamoto inayoiwezesha kupata fikra mbadala na viongozi wenye misimamo na mitazamo mipya na inayobadilika na wakati.
Kazi zao nyingi hazina usaidizi wa aina yoyote ile ukiwa ule wa zana, fedha au rasilimali watu. Na kwa hiyo, kwa wakati mwingi ni sehemu ndogo ya yale yaliyostahili kuwa majukumu yao yanatekelezwa kikamilifu.
Wrengi wanajiona wanatumika zaidi kisiasa na baadhi yao wanaamini pengine kile walichostahili kulipwa huliwa na wale walio juu yao. Zaidi ya hilo mara chache sana maamuzi yana sauti katika masuala mbalimbali. Kwa hiyo huiona zaidi ni yoyo kuliko watu wenye sauti katika mambo mengi yanayowazunguka. Nafuu kwao huja wakati wa chaguzi kwani ndipo wanapoweza kupambanisha pande mbalimbali na kuzikamua angalau wapate maziwa ya watoto.
Huu ni wakati mzuri wa kujiuliza, hivi, kama viongozi wa ngazi za chini wangekuwa na elimu, maarifa na uono sawa na wale wa juu majimbo yetu ya uchaguzi yangelikuwa kama hivi yalivyo. Na, je ni mtaji kwa serikali kwa wananchi vijijini kuwa mbumbumbu wa faida za siasa za ushindani ? Na wabunge tunaowapata kwa mfumo huu wa sasa wangelikuwa ndio hao hao katika mazingira ambayo kuna wasomi kushinda wao katika ngazi za uongozi wa chini ?
Ni rahisi kuelewa kwa nini hakuna anayetaka kugombea nafasi za kuwa mjumbe wa nyumba kumi au balozi au diwani au mwenyekiti wa serikali ya mtaa. Kwa upande mwingine kila mtu anataka kugombea ubunge, uwakilishi na urais. Hata hao waliopo asilimia 80 ya muda wao hutumika kujitafutia riziki kwingineko na ni kama asilimia 20 tu ndiyo hutumika kuangalia mambo ya wananchi/serikali.
Kutokana na ukweli huu kwamba kuna mfumo na hali ambayo inasababisha watu watake kugombea ubunge, uwakilishi na urais lakini hakuna wanaotaka kugombea ubalozi wa mitaa au uenyekiti wa mtaa ni dhahiri kuwa ipo haja ya kuleta mapinduzi makubwa ya uongozi katika ngazi za chini ikiwa kama kweli tunataka tujikwamue na hali hii ya kuwa masikini wakubwa duniani. Na uongozi wowote (uwe wa chini au wa juu) lazima uwe ni kazi au tarafu inayolipwa kima mahsusi kinachowawezesha viongozi hao wote kujitoa kwa hali na mali kutimiza zaidi majukumu yao ya kikazi kuliko ya kibinafsi.
Tuanze na utafiti na ushauri
Ninapendekeza kuwa Chuo Kikuu cha Mzumbe kikishirikiana na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania chenye tawi karika kila mkoa waanze kwa utafiti na ushauri katika kila mkoa kuona ni namna gani tunavyoweza kuongeza hatua kwa hatua, ubora wa viongozi waliopo na wakati huo huo kuwashawishi watu wenye uwezo, elimu na ujuzi zaidi kukubali kuwa wajumbe wa nyumba kumi na viongozi wa serikali za mitaa. Bila kuwasahau madiwani wetu. Baada ya kazi za utafiti na ushauri yaanze mafunzo na uandaaji wa mipango ya urithishaji uongozi kwa namna ambayo kila mtaa, kila kata inapata kiongozi anayestahili kushika nafasi hiyo.
Ninaamini ya kwamba, masomo kama vile yale ya uchumi, uongozi( leadership) utawala (governance) , uangalizi wa fedha, menejimenti, sayansi ya jamii, usimamizi rasilimali watu, mipango, udhibiti, sayansi ya maamuzi na kadhalika hayatakosekana na yatatolewa kwa lugha mama ya Watanzania, yaani, Kiswahili.
Thursday, July 15, 2010
Mahakama ya Rufaa imethibitisha Katiba Mpya yahitajika ...
WAKATI wananchi wa Kenya karibuni watapigia kura pendekezo la Katiba mpya nchini mwao, Tanzania, nchi iliyoitangulia Kenya katika kukubali demokrasia ya kisiasa haijaona umuhimu wa kuwa na katiba mpya licha ya mapungufu mengi ambayo watu wengi nikiwemo na mimi tumekwishaonesha mapungufu yake kadhaa. Kwa kifupi katiba tuliyo nayo haitofautiani na kutumia taipureta katika karne ya kompyuta.
Hata hivyo, masuala kadhaa yaliyozuka ndani na nje ya nchi kwa hivi sasa yanaashiria kuonesha kuwa kukataa katiba mpya nchini Tanzania ni jambo ambalo linakaribia kupoteza sababu na mantiki katika kila nyanja ya maisha, siasa na kazi.
Mathalani, kadhia ya mgombea huru na jinsi mhimili wa sheria ulivyoterereka na kukwepa wajibu wake umeonesha wazi kwamba bila ya kuwa na katiba mpya jambo hili litafanywa kwa mizengwe na matakwa ya chama tawala na sio kisheria wala kidemokrasia. Hii ni kusema ipo hatari kubwa ya nchi kuendelea kuongozwa kutokana na haja na matakwa ya mtu au watu badala ya kuwa na mifumo hai inayofanya kazi bila kuingiliwa na utashi wa mtu katika maeneo mbalimbali ya utawala na uongozi wa nchi.
Katiba iliyopo sasa inakubali na kuamini katika uhuru usiokuwa na kikomo ndani ya sheria za nchi. Wanachokitaka wengine ni kuweka mipaka kwa uhuru wa Mtanzania, hususan ule wa kuchagua na kuchaguliwa ndani au nje ya chama cha kisiasa.
Tukio lingine ni lile la kupitishwa kwa itifaki ya soko la pamoja la Afrika Mashariki. Inaelekea Tanzania imekutwa katika hali ya kuwa bado imeshusha kaptula yake na inataka faragha ya muda kujiweka sawa. Badala ya mambo haya, hata kufanyika kwa msaada wa ushauri na utafiti wa wasomi wetu, wataalamu na mabingwa wa nyanja mbalimbali, inaelekea yanafanyika bado kisiasa na matakwa ya watu fulani ikidhihirisha kuwa hata tukipewa miaka 20 hatutaweza kubadili chochote. Kusahihisha jambo hili ni lazima pawe na katiba mpya na itakayobainisha waziwazi ni kwa kiasi gani nchi hii itatoa ruhusa ya kumegua uhuru wake katika kutafuta umoja wa Afrika Mashariki na Afrika nzima kwa ujumla. Ni lazima tuwe na katiba inayoona mbali kwa miaka hata zaidi ya hamsini. Sio katiba iliyoishia katika uhuru na Azimio la Arusha.
Kuna wanaoamini kwamba Tanzania haiwezi kuendelea kama kila kitu kitakuwa kinaamuliwa kutoka Dar es salaam. Jamaa hao wanaamini ipo haja ya kuwa na mikoa huru kiuchumi na kijamii kama tunataka kuendelea kwa uhakika na haraka zaidi. Tishio kwa umoja kupitia ukabila hivi sasa sio kubwa kama tishio la ukabila wa kichama. Je, uziro wa jambo hili haulifanyi kuwa katika katiba mpya ?
Wakati Zanzibar ina mahakama ya Kadhi kama ilivyo kwa Kenya na Uganda na suala hili limo katika Katiba ya nchi zao na ambazo ukitoa Zanzibar ni nchi zenye wakiristo wengi zaidi kuliko Waislamu chama tawala hapa nchini kimefikia uamuzi wa kukataa mahakama ya kadhi isiwemo katika katiba kinyemela. Jambo linaloacha ufa wa kutisha siku zijazo za Waislamu wenye siasa kali kwenda njia nzima na kuwa na shariya maana hawakujumlishwa na usaikula eti kwa kisingizio cha kuogopa gharama ambazo zinatumika kwa wananchi wale wale wanaochangia hazina ya taifa kwa kodi na matumizi yao mbalimbali. Uamuzi huu unakuwa sio tu undumilakuwili bali pia ni wenye kuning'inia kwa kamba ya shinikizo za nje na hauashirii mahusiano mema kati ya imani zetu za kidini katika miaka ijayo. Hili sio jambo la kutania, na watu wachache kwa shinikizo yoyote ile isikubaliwe wafikie maamuzi ambayo kizazi cha baadaye kitakuja kuyajutia. Ni lazima suala hili litambulike kikatiba na sio vinginivyo.
Sehemu kubwa ya Waislamu hawaitambui BAKWATA, lakini kwa sababu moja au nyingine serikali bado inashinikiza kuwa BAKWATA peke yake ndio mwakilishi halali wa Waislamu. Hii sio bishara njema, ni lazima pawepo na katiba mpya ili kudhihirisha wazi uhuru wa kila dini kujiundia wenyewe vyombo vya kuwawakilisha katika masuala mbalimbali. Taasisi inayoonekana kufadhiliwa na kulindwa na serikali haiwezi kukubalika kuwa mwakilishi halali wa wanaimani wanaohusika.
Kuna wanaoamini kwamba vyombo vya habari vya serikali ni mzigo kwa walipa kodi usio wa lazima, j e, hili halioneshi kwamba ipo haja ya katiba mpya ambayo pamoja na mambo mengine itaangalia pia
nini uwe uhusiano wa vyombo vya habari, na serikali; vyombo hivyo na vyama vya siasa na vyombo hivyo na wananchi ? Kwa wengi, vyombo hivi kama vilivyo vingi vinginevyo vinaonekana ni mianya kwa baadhi ya watu na taasisi kula fedha za umma bila ya wachungaji kupiga mayowe na wakati mwingine bila kujua.
Dai mojawapo kubwa la vyama mbadala nchini ni kuwepo kwa tume huru. Tume itakayokuwa haiegemei upande wowote na hivyo kusimamia chaguzi zitakazokuwa huru. Je, ni kwa kiasi gani hili linaweza kukamilika bila ya kuwa na katiba mpya ?
Toka tupate uhuru azma moja yetu kubwa ilikuwa ni kupunguza tofauti kati ya miji na vijiji, wakulima na wafanyakazi, matajiri na maskini je, hili, limefanikiwa kwa kiasi gani. Hivi 'apartheid kati ya miji na vijiji' inaweza kuondoka bila ya kuwepo kwa katiba mpya ?
Kuna watu wa makabila mbalimbali nchini ambao wanaamini kwamba redio zingelikuwa zinatangaza kwa lugha za makabila yao basi sio tu wangelihabarika, kuelimika na kustareheka zaidi lakini mapambano yao ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii yangelikuwa rahisi zaidi. Lakini sheria na katiba iliyopo havielekei kuoana katika kauli za kama iwepo au isiwepo ruhusa. Isitoshe wanasiasa wa kale lakini wasiothamini utu na utamaduni wetu hawalikubali hili. Wanaleta hofu ya bure ambayo inastahili sasa kuwa dhidi ya wanasiasa wenye ubaguzi wa kichama nchini. Nchi kwa hiyo inatawaliwa kwa uoga badala ya hoja za msingi zenye mantiki inayokubalika.
Habari za mama na mabinti wetu kujifungua barabarani na chini ya miti haziachi kusikika toka huku na kule. Madaktari na manesi wetu wanalaumiwa kwa roho mbaya lakini hili linaanzia kwenye mishahara mibaya. Je, bado kweli hatujaona haja ya kuwa na kipengele ndani ya katiba mpya kinachozungumzia kwa kina ni nini iwe sera ya afya kwa wananchi wetu-wenye nacho na wasio nacho daima dawamu ? Haisemi lolote jinsi ya kuboresha hospitali hizo ili ziweze kutibu wanaopelekwa nje kutibiwa na vilevile kutibu wagonjwa kutoka nje na nafuu inayopatikana iwe ni nafuu itakayoweza kutoa tiba ya bure kwa watu masikini.
Kuna suala la usafi, mipango miji na utunzaji mazingira mijini na vijijini ambalo hata hapa Dar es salaam wanapoishi wakubwa linaelekea sio tu halina mwenyewe bali hakuna viwango vya kumzawadia mtu zabuni ya kusafisha mji na matokeo ya hili ni kuwa msafisha mji na vyombo wanalitia jiji uchafu na sura mbaya zaidi, je, halistahili nalo kusahihishwa na katiba mpya ? Na katiba hiyo haiwezi kwenda mbali na kutangaza rasmi maadili ya Watanzania kama yatakavyokubalika na walio wengi.
Suala la madini nigodi pamoja na kuwepo na sera mpya bado linastahili kuingizwa ndani ya katiba kwa namna ambayo watu na madini yetu yataonekana kuwa na thamani zaidi kuliko wawekezaji na mitambo yao na vizawadi vya barabara, shule na zahanati wanavyotudanganya navyo. Zanzibar inadai mafuta ni yake wakubwa bara wanasema mafuta ni yetu. Tumfuate nani? Dawa hapa hivi kweli siyo katiba iliyo wazi juu ya jambo hili ?
Kuna wanaoamini kuwa mashirika kama yale ya hifadhi za jamii yanastahili kwa kiasi kikubwa kumilikiwa na wanachama wenyewe na sio na serikali na wanasiasa. Wanadai umilikaji wa sasa hivi unawanyonya na kuwapunja wanachama kwa njia nyingi. Makato ya mwanachama yakigeuzwa ni hisa ndani ya mashirika hayo wanachama watafaidika zaidi kuliko ilivyo hivi sasa. La, sivyo, basi pawe na uhuru wa kuanzisha hifadhi huru za jamii kwa kila tarafu.
Kuna wanaoamini, Tanzania yenye viongozi wanaotaka kweli kuwaondoa wananchi wake toka kwenye umaskini ina uwezo kwa kutumia rasilimali zake yenyewe kujengea kila familia nchini, mjini na vijijini angalau nyumba ya vyumba viwili. Jambo hili sio tu litazusha ajira kubwa na pato kubwa kwa nchi na watu wake bali pia litaondosha aibu ya kila Mtanzania kuwa na mradi wa kujenga nyumba ya kuishi badala ya kujenga biashara au kiwanda.
Hata hivyo, masuala kadhaa yaliyozuka ndani na nje ya nchi kwa hivi sasa yanaashiria kuonesha kuwa kukataa katiba mpya nchini Tanzania ni jambo ambalo linakaribia kupoteza sababu na mantiki katika kila nyanja ya maisha, siasa na kazi.
Mathalani, kadhia ya mgombea huru na jinsi mhimili wa sheria ulivyoterereka na kukwepa wajibu wake umeonesha wazi kwamba bila ya kuwa na katiba mpya jambo hili litafanywa kwa mizengwe na matakwa ya chama tawala na sio kisheria wala kidemokrasia. Hii ni kusema ipo hatari kubwa ya nchi kuendelea kuongozwa kutokana na haja na matakwa ya mtu au watu badala ya kuwa na mifumo hai inayofanya kazi bila kuingiliwa na utashi wa mtu katika maeneo mbalimbali ya utawala na uongozi wa nchi.
Katiba iliyopo sasa inakubali na kuamini katika uhuru usiokuwa na kikomo ndani ya sheria za nchi. Wanachokitaka wengine ni kuweka mipaka kwa uhuru wa Mtanzania, hususan ule wa kuchagua na kuchaguliwa ndani au nje ya chama cha kisiasa.
Tukio lingine ni lile la kupitishwa kwa itifaki ya soko la pamoja la Afrika Mashariki. Inaelekea Tanzania imekutwa katika hali ya kuwa bado imeshusha kaptula yake na inataka faragha ya muda kujiweka sawa. Badala ya mambo haya, hata kufanyika kwa msaada wa ushauri na utafiti wa wasomi wetu, wataalamu na mabingwa wa nyanja mbalimbali, inaelekea yanafanyika bado kisiasa na matakwa ya watu fulani ikidhihirisha kuwa hata tukipewa miaka 20 hatutaweza kubadili chochote. Kusahihisha jambo hili ni lazima pawe na katiba mpya na itakayobainisha waziwazi ni kwa kiasi gani nchi hii itatoa ruhusa ya kumegua uhuru wake katika kutafuta umoja wa Afrika Mashariki na Afrika nzima kwa ujumla. Ni lazima tuwe na katiba inayoona mbali kwa miaka hata zaidi ya hamsini. Sio katiba iliyoishia katika uhuru na Azimio la Arusha.
Kuna wanaoamini kwamba Tanzania haiwezi kuendelea kama kila kitu kitakuwa kinaamuliwa kutoka Dar es salaam. Jamaa hao wanaamini ipo haja ya kuwa na mikoa huru kiuchumi na kijamii kama tunataka kuendelea kwa uhakika na haraka zaidi. Tishio kwa umoja kupitia ukabila hivi sasa sio kubwa kama tishio la ukabila wa kichama. Je, uziro wa jambo hili haulifanyi kuwa katika katiba mpya ?
Wakati Zanzibar ina mahakama ya Kadhi kama ilivyo kwa Kenya na Uganda na suala hili limo katika Katiba ya nchi zao na ambazo ukitoa Zanzibar ni nchi zenye wakiristo wengi zaidi kuliko Waislamu chama tawala hapa nchini kimefikia uamuzi wa kukataa mahakama ya kadhi isiwemo katika katiba kinyemela. Jambo linaloacha ufa wa kutisha siku zijazo za Waislamu wenye siasa kali kwenda njia nzima na kuwa na shariya maana hawakujumlishwa na usaikula eti kwa kisingizio cha kuogopa gharama ambazo zinatumika kwa wananchi wale wale wanaochangia hazina ya taifa kwa kodi na matumizi yao mbalimbali. Uamuzi huu unakuwa sio tu undumilakuwili bali pia ni wenye kuning'inia kwa kamba ya shinikizo za nje na hauashirii mahusiano mema kati ya imani zetu za kidini katika miaka ijayo. Hili sio jambo la kutania, na watu wachache kwa shinikizo yoyote ile isikubaliwe wafikie maamuzi ambayo kizazi cha baadaye kitakuja kuyajutia. Ni lazima suala hili litambulike kikatiba na sio vinginivyo.
Sehemu kubwa ya Waislamu hawaitambui BAKWATA, lakini kwa sababu moja au nyingine serikali bado inashinikiza kuwa BAKWATA peke yake ndio mwakilishi halali wa Waislamu. Hii sio bishara njema, ni lazima pawepo na katiba mpya ili kudhihirisha wazi uhuru wa kila dini kujiundia wenyewe vyombo vya kuwawakilisha katika masuala mbalimbali. Taasisi inayoonekana kufadhiliwa na kulindwa na serikali haiwezi kukubalika kuwa mwakilishi halali wa wanaimani wanaohusika.
Kuna wanaoamini kwamba vyombo vya habari vya serikali ni mzigo kwa walipa kodi usio wa lazima, j e, hili halioneshi kwamba ipo haja ya katiba mpya ambayo pamoja na mambo mengine itaangalia pia
nini uwe uhusiano wa vyombo vya habari, na serikali; vyombo hivyo na vyama vya siasa na vyombo hivyo na wananchi ? Kwa wengi, vyombo hivi kama vilivyo vingi vinginevyo vinaonekana ni mianya kwa baadhi ya watu na taasisi kula fedha za umma bila ya wachungaji kupiga mayowe na wakati mwingine bila kujua.
Dai mojawapo kubwa la vyama mbadala nchini ni kuwepo kwa tume huru. Tume itakayokuwa haiegemei upande wowote na hivyo kusimamia chaguzi zitakazokuwa huru. Je, ni kwa kiasi gani hili linaweza kukamilika bila ya kuwa na katiba mpya ?
Toka tupate uhuru azma moja yetu kubwa ilikuwa ni kupunguza tofauti kati ya miji na vijiji, wakulima na wafanyakazi, matajiri na maskini je, hili, limefanikiwa kwa kiasi gani. Hivi 'apartheid kati ya miji na vijiji' inaweza kuondoka bila ya kuwepo kwa katiba mpya ?
Kuna watu wa makabila mbalimbali nchini ambao wanaamini kwamba redio zingelikuwa zinatangaza kwa lugha za makabila yao basi sio tu wangelihabarika, kuelimika na kustareheka zaidi lakini mapambano yao ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii yangelikuwa rahisi zaidi. Lakini sheria na katiba iliyopo havielekei kuoana katika kauli za kama iwepo au isiwepo ruhusa. Isitoshe wanasiasa wa kale lakini wasiothamini utu na utamaduni wetu hawalikubali hili. Wanaleta hofu ya bure ambayo inastahili sasa kuwa dhidi ya wanasiasa wenye ubaguzi wa kichama nchini. Nchi kwa hiyo inatawaliwa kwa uoga badala ya hoja za msingi zenye mantiki inayokubalika.
Habari za mama na mabinti wetu kujifungua barabarani na chini ya miti haziachi kusikika toka huku na kule. Madaktari na manesi wetu wanalaumiwa kwa roho mbaya lakini hili linaanzia kwenye mishahara mibaya. Je, bado kweli hatujaona haja ya kuwa na kipengele ndani ya katiba mpya kinachozungumzia kwa kina ni nini iwe sera ya afya kwa wananchi wetu-wenye nacho na wasio nacho daima dawamu ? Haisemi lolote jinsi ya kuboresha hospitali hizo ili ziweze kutibu wanaopelekwa nje kutibiwa na vilevile kutibu wagonjwa kutoka nje na nafuu inayopatikana iwe ni nafuu itakayoweza kutoa tiba ya bure kwa watu masikini.
Kuna suala la usafi, mipango miji na utunzaji mazingira mijini na vijijini ambalo hata hapa Dar es salaam wanapoishi wakubwa linaelekea sio tu halina mwenyewe bali hakuna viwango vya kumzawadia mtu zabuni ya kusafisha mji na matokeo ya hili ni kuwa msafisha mji na vyombo wanalitia jiji uchafu na sura mbaya zaidi, je, halistahili nalo kusahihishwa na katiba mpya ? Na katiba hiyo haiwezi kwenda mbali na kutangaza rasmi maadili ya Watanzania kama yatakavyokubalika na walio wengi.
Suala la madini nigodi pamoja na kuwepo na sera mpya bado linastahili kuingizwa ndani ya katiba kwa namna ambayo watu na madini yetu yataonekana kuwa na thamani zaidi kuliko wawekezaji na mitambo yao na vizawadi vya barabara, shule na zahanati wanavyotudanganya navyo. Zanzibar inadai mafuta ni yake wakubwa bara wanasema mafuta ni yetu. Tumfuate nani? Dawa hapa hivi kweli siyo katiba iliyo wazi juu ya jambo hili ?
Kuna wanaoamini kuwa mashirika kama yale ya hifadhi za jamii yanastahili kwa kiasi kikubwa kumilikiwa na wanachama wenyewe na sio na serikali na wanasiasa. Wanadai umilikaji wa sasa hivi unawanyonya na kuwapunja wanachama kwa njia nyingi. Makato ya mwanachama yakigeuzwa ni hisa ndani ya mashirika hayo wanachama watafaidika zaidi kuliko ilivyo hivi sasa. La, sivyo, basi pawe na uhuru wa kuanzisha hifadhi huru za jamii kwa kila tarafu.
Kuna wanaoamini, Tanzania yenye viongozi wanaotaka kweli kuwaondoa wananchi wake toka kwenye umaskini ina uwezo kwa kutumia rasilimali zake yenyewe kujengea kila familia nchini, mjini na vijijini angalau nyumba ya vyumba viwili. Jambo hili sio tu litazusha ajira kubwa na pato kubwa kwa nchi na watu wake bali pia litaondosha aibu ya kila Mtanzania kuwa na mradi wa kujenga nyumba ya kuishi badala ya kujenga biashara au kiwanda.
Subscribe to:
Posts (Atom)
