MBONA mimi siwaelewi hawa Wazungu! Eti wanasema hakuna kazi. Ajira sasa ni ngumu? Hivi ni kweli ? Ninavyoona mimi ni kuwa jamaa hawa wanaonesha tu ubinafsi jambo ambalo kwa kawaida wamelizoea. Ajira zipo tena kabakaba. Hebu jiulize:
. Hakuna barabara na madaraja ya kujenga Afrika ?
. Waafrika wangapi wanaishi katika nyumba zinazostahili kuitwa nyumba ?
. Je tuna madaktari wa kutosha Afrika ?
. Je, tuna walimu wa kutosha Afrika ?
. Je asilimia ngapi ya watu wetu wanapata umeme na maji safi ? Ongeza na maswali mengine kiasi utakacho na majibu utakayopata ni kwamba ajira kwa wazungu wote wasio na ajira na wanaotaka kuja kufanya kazi ili kuijenga Afrika zipo. Tatizo ni ubinafsi wa Viongozi wao ambao wanasema heri wawalipe watu wao mshahara bila kufanya kazi kuliko waje kuijenga Afrika ? Na hicho wanacholipwa hivi kweli hakijaibiwa na wachimba dhahabu na almasi na madini mengine watokao Marekani, Canada na Australia ?
Ajira ipo, ila ubinadamu na utu hamna!
Thursday, May 28, 2009
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

No comments:
Post a Comment